Askofu Bagonza aibuka na mambo matatu, ' nimejizuia kuandika kusema chochote Lakini mmenisonga'

  Рет қаралды 3,001

Mwananchi Digital

Mwananchi Digital

11 ай бұрын

Baada ya mkutano mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) kumalizika kwa kupata Mkuu wa kanisa hilo mpya, Askofu wa Dayosisi ya Karagwe, Benson Bagonza ameibuka na mambo matatu.
Askofu Bagonza ameeleza mambo hayo baada ya juzi usiku Alhamisi Agosti 24,2023 kuhitimishwa kwa uchaguzi ambapo Askofu Alex Malasusa wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani kuibuka mshindi wa Mkuu wa KKKT akichukua nafasi iliyoachwa na Askofu Fredrick Shoo aliyemaliza muda wake wa uongozi.
Askofu huyo ametumia kurasa zake za kijamii, kuandika ujumbe wenye mambo matatu ya kufikirisha akiupa kichwa cha habari 'hatugombei, tunagombezwa.'
Ujumbe huo wa Askofu Bagonza unasema:
Wapendwa wangu, nimejizuia sana kuandika au kusema chochote. Lakini mmenisonga sana, nami nimo safarini. Kwa kuwa sijui kama nitafika niendako (Vienna) kabla hamjakata tamaa na kuzimia, naomba msome kwa furaha mambo haya matatu:
1. Tumetazamwa na dunia nzima kwa siku nne. Mmoja aliyeona na alikuwa mgeni akaniuliza: “Hivi nyie wenzetu Wachungaji na Maaskofu mmeishagundua mbingu haipo mkafanya iwe siri yenu tu?” Akaongeza, “kama mbingu ipo kwa nini mfanyiane haya mabaya hadharani?
2. Nilizoezwa kuamini kuwa watu wanakataliwa kwa sababu ya ubaya wao na wengine hupendwa kwa sababu ya uzuri wao. Sasa nimeamini wapo wanaoweza kukataliwa kwa uzuri na wakapendwa kwa ubaya wao. Cha msingi, ubaya hauwezi kukaa kwa amani na wema. Tumefundishwa:
Katika Agano la Kale, kichafu kikigusana na kitakatifu, kile kitakatifu kinaharibika.
Katika Agano Jipya, kichafu kikigusana na kitakatifu, kile kichafu kinatakasika. TKKK ni ya Agano Jipya au la Kale?
3. Watu wakatili na waovu hujiandaa kupiga na kuangamiza wabaya wao wakati wote. Watu wema hutafuta kuushinda ubaya kwa wema.
Hutokea wakati, wapigaji wakapiga na kufurahi kuwa wamepiga. Wakitulia hugundua kuwa kumbe wamepigwa sana. Kutosamehe ni sawa na kunywa sumu ukitegemea afe adui yako. Sumu uliyokumywa bila kukusudia inaua vibaya.
Humu kibandani kwetu huwa hatugombei bali tunagombezwa na kuzodolewa.
Unione nitakapokuona.

Пікірлер: 9
@user-rs4vz2vt9z
@user-rs4vz2vt9z 11 ай бұрын
Bwana yesu alisema nakwenda kuanda makao kisha nitakuja kuwachukua sio twende tukamchukue,tukiendelea hivi iko siku watu watapanga kwenda kumchukua Yesu.zaidi ya maaskofu mia mbili mmekosa mkuu mpya mpaka mumchue mkuu mstahafu!!!!!!!!!!!!,ni mara chache sana kura ilitenda haki.Wakatoliki mungu awabariki.
@geraldadolf4928
@geraldadolf4928 11 ай бұрын
Kiukweli mmezingua sana
@Bennymwangaza
@Bennymwangaza 11 ай бұрын
Matendo ya Mitume 1:26 [26]Wakawapigia kura; kura ikamwangukia Mathiya; naye akahesabiwa kuwa pamoja na mitume kumi na mmoja.
@user-rs4vz2vt9z
@user-rs4vz2vt9z 11 ай бұрын
@@Bennymwangaza kwenye matendo ya mitume aliye chaguliwa Alishawahi kuwa mtume,?,kwanini asiwekwe pembeni ambao hawaja wahi kua wachaguliwe,au kuna some thing behind.
@Bennymwangaza
@Bennymwangaza 11 ай бұрын
@@user-rs4vz2vt9z HAPO NAKUBALIANA NA HOJA YAKO KWENYE JAMBO LA KUJIRUDIA SIO SAHIHI LKN MM NILIKUA NAKUWEKA SAWA KWENYE *KURA*
@user-rs4vz2vt9z
@user-rs4vz2vt9z 11 ай бұрын
@@Bennymwangaza Ni sawa ndugu Ila hawa viongozi wa kanisa wamekua kama kanisa ni lao si LA mungu,kwahiyo wanafanya wanavyotaka,ndio maana nikasema kati ya maaskofu zaidi ya mia mbili hakupatikana mtu?,sisi waumini tunajenga makanisa kwa hela zetu tunajitoa hata Mali zetu kwa ajili ya kanisa,kwanini wasimtangulize mungu kwenye jambo kubwa kama hili na sio maslai binafsi au ya watu Fulani.mahali popote kweli ikiondoka uovu unatawala.
@daffagunda-rm3hj
@daffagunda-rm3hj 11 ай бұрын
Always natural follow the natural.Amen
Ni kuri na njira njeru cia kweheria Rigathi Gachagua wabici-ini.
27:06
KAMEME OFFICIAL PAGE
Рет қаралды 1,3 М.
Jumping off balcony pulls her tooth! 🫣🦷
01:00
Justin Flom
Рет қаралды 28 МЛН
Mama vs Son vs Daddy 😭🤣
00:13
DADDYSON SHOW
Рет қаралды 50 МЛН
Secret Experiment Toothpaste Pt.4 😱 #shorts
00:35
Mr DegrEE
Рет қаралды 38 МЛН
Mom's Unique Approach to Teaching Kids Hygiene #shorts
00:16
Fabiosa Stories
Рет қаралды 38 МЛН
“Viongozi wa Dini tumepoteza ushawishi” -Askofu Bagonza
5:47
Jumping off balcony pulls her tooth! 🫣🦷
01:00
Justin Flom
Рет қаралды 28 МЛН