Рет қаралды 41,426
Baba mzazi wa Beneth Kiwelu ambaye alikuwa mwanafunzi wa shule ya msingi Mount Sayuni, Laurence Kiwelu amesema mwanae hakufariki kwa kupigwa na mwalimu bali alikuwa akisumbuliwa na magonjwa mengine.
Kiwelu ameyasema hayo katika mahojiano aliyofanya na Mwananchi Digital muda mchache tangu kusambaa kwa taarifa za kifo cha mwanae huku sababu kubwa ikitajwa kuwa kipigo kutoka kwa mwalimu kilichomfanya alazwe katika chumba cha uangalizi maalumu (ICU).