Рет қаралды 19,458
Mbunge wa Jimbo la Konde (ACT Wazalendo), Mohamed Said Issa amesema msimamo wake kuhusu watu kwenda Zanzibar kwa paspoti bado uko vilevile isipokuwa awali watu wengi hawakuelewa maneno yake lakini alichokimaanisha ni kuweka paspoti kwa lengo la kuvilinda visiwa hivyo.
Mohamed ameyasema hayo leo Jumanne, Mei 7, 2024 alipozungumza na Mwananchi Digital Bungeni jijini Dodoma ambapo amesema kumekuwa na watu wengi ambao wamekuwa wakienda Zanzibar kutoka mataifa ya jirani bila paspoti kwasababu ya utaratibu uliopo sasa hivi.
Aidha katika mahojiano haya Mbunge huyu pia ameeleza kuwa angetamani Watanzania wote wapewe pasi za kusafiria punde wanapozaliwa ili kurahisisha usafiri kwenda maeneo mbalimbali pamoja na kulinda visiwa vya Zanzibar kwani utaratibu huo unatumika nchini Uchina pamoja na Uingereza.