No video

FAHAMU MAZINGIRA YA PAROKIA YA MTAKATIFU ANTONY WA PADUA MBAGALA ZAKHIEM - KANISA NA MALIMWENGU

  Рет қаралды 11,705

Jugo Media

Jugo Media

Күн бұрын

HISTORIA FUPI YA PAROKIA YA MT. ANTHONY WA PADUA
MBAGALA- ZAKHEM
Parokia ya Mbagala iliyoanzishwa mwaka 1954 ikiwa ni mojawapo kati ya Parokia kongwe katika Jimbo Kuu la Dar Es Salaam. Kipindi hicho Jimbo kuu la Dar lilikuwa pamoja na Vicariet ya Jimbo la Mahenge likiongozwa na Hayati Askofu Edgar Marantha.
Parokia ya Mbagala ilianzishwa katika eneo ambalo sasa ni kituo cha kiroho (Mbagala spiritual Centre) eneo la Parokia lilikuwa kubwa ambalo ni kusini mashariki ya Jimbo kuu la Dar Es Salaam kuanzia Mbagala hadi Kilwa Kipatimu; kwa sasa ni eneo la Parokia za Kizuiani, Kijichi, Kizinga, Mbagala Kuu, Mbande, Kongowe, Toangoma, Vikindu, Mkuranga, KisijuPwani, Kibiti na baadhi za Parokia za Jimbo la Lindi.
Parokia hii tangu kuanzishwa kwake imekuwa ikihudumiwa na mapadre na watawa wa Shirika la Wafransiskani Wakapuchini. Mwaka 1984 Parokia ya Mt. Anthony wa Padua ilihamishiwa eneo la Mbagala Zakhem kufuatia kupatikana kwa eneo hilo na mahitaji ya kuanzishwa kwa kituo cha kiroho na baadaye nyumba ya watawa wadada wadogo.
Parokia yetu imejaliwa kuwa na mashirika ya watawa wanawake matano ambayo ni Masista Wafransisko Utawala wa Bwana, Masista wa Holy Union, Masista wa Mkombozi, Masista Wakamaldolesi na Masista Wabenediktini wa Chipole. Mashirika haya yamekuwa chachu ya uinjilishaji na pia msaada mkubwa katika huduma za kijamii katika Parokia yetu.
Tangu mwaka 1954 hadi 2018 Parokia ya Mbagala imepitia hatua mbali mbali za kukua kimwonekano, kiimani na kimaendeleo ikiwa ni pamoja na kuzaliwa kwa Dekania za Kigamboni na Kilimahewa zenye zaidi ya Parokia 17.
Parokia imesimamia uanzishwaji wa parokia mpya kadhaa ambazo zilihitaji miundo mbinu mipya ili kupata sifa za kuteuliwa kuwa parokia, michango ya waumini, ufadhili na msaada kutoka kwa Jimboni ilifanikisha miradi kukamilika kwa wakati na kupata nafasi ya kuanza mingine mipya.
Mapadre wanaohudumia parokia ya Mbagala Zakhem kwa sasa ni:-
1. Raphael Henry Chiligwalwa (paroko) 0754 563 639
2. Nolascus Charles Mwandambo 0756630684/0655 630 684
3. Prosper Anthony Kessy 0755 444 471
Tunashukuru Mungu kwa zawadi ya mapadre wa shirika la Ndugu wadogo wa Wafransiscani Wakapuchini kwa huduma zao kwenye Parokia yetu, ambao wanatupa huduma zote kwa kadri ya mahitaji na maelekezo ya Kanisa Katoliki.

IDADI YA WAAMINI
Parokia ya Mbagala Zakhem in jumla ya waamini 12,250 kutokana na sensa ya mwaka 2018 wanaotoka katika kanda 42 na jumuia 118 ambazo zinaunda vigango vitatu vya Chamazi, Vigoa na MajiMatitu. Ndani yake kuna kituo cha sala kimoja; Vigozi kilichopo eneo la Mponda, Parokiani.
i. Waamini wanaozunguka eneo la Parokia wako katika kanda 24 na jumuia 63 zenye jumla ya waamini 5,719. ii. Waamini wanaozunguka kigango cha Maji matitu wako katika kanda 5 zenye jumla ya Jumuia 12 na waamini 1,265
iii. Waamini wanaozunguka kigango cha Chamazi wako katika kanda 13 zenye jumla ya Jumuia 43 na waamini 5266.

Parokia yetu naweza kusema haijaishiwa na shughuli za maendeleo ikiwemo ujenzi katika vigango vyetu na vituo vya sala. Waamini wamekuwa msingi wa miradi yote hiyo tunawashukuru sana.
Mawasiliano:
JUGO MEDIA,
Sokoine Drive, Posta
P. O. BOX 34014,
Dar es Salaam.
For Bookings and other Enquiries
Phone Number +255757560764/657790405
#jugomedia #kanisakatoliki #familiatakatifu #wawata #uwaka #viwawa

Пікірлер: 32
@avelinaaudax4672
@avelinaaudax4672 Жыл бұрын
Hongereni sana.Mungu azidi kuwapigania kweli pemependeza sana.nimesali sana hapo na kuimba kwaya miaka ya 1996.hakika kumebadilika sana.
@mary-stellakivali8872
@mary-stellakivali8872 3 жыл бұрын
Baba paroko tumsifu Yesu kristu. Asante sana kwa tour ya kwenye parokia yako na ni nzuri sana. Hongereni kwa kazi nzuri. Naomba nitoe wazo moja kama mngeweza kufungwa na kituo cha kutunza wazee kama wenzetu wa huku ughaibuni kwa gharama yoyote ingekuwa kitega uchumi kizuri na wazazi wetu sisi tuliopo huku ughaibuni wangepata uangalizi wenye kuaminika. Haya tunayaona huku kwenye nchi za wenzetu na watu wengi wamepata ajira humo kwenye hizo Residential homes. Ubarikiwe sana
@helencyprian8745
@helencyprian8745 8 ай бұрын
Hongera sana Fr Kesy
@vicentmigodela190
@vicentmigodela190 2 жыл бұрын
Mazingira mazuri mnoooo! Wakatoriki mnajitahidi Sana kutumia sadaka za waamini wenu vizuri.inatia moyo Sana ya kutoa sadaka kwasababu Kazi inaonekana
@cleversanga7791
@cleversanga7791 Жыл бұрын
Mungu awabariki Sana Wana parokia wote kwa ujumla
@dinnamlwilo3795
@dinnamlwilo3795 4 жыл бұрын
Kwa kweli Parokia ya Mbagala imebadilika hongereni sana na Mungu awaendelee kuwalinda
@deogratiasfabianbangana3410
@deogratiasfabianbangana3410 3 жыл бұрын
Mungu akubariki fadher prosper kwa ukandalasi mzuri ambuo mungu amekujalia,,,,
@johnb.j.m206
@johnb.j.m206 3 жыл бұрын
Hongera sana Ndugu pamoja na waamini wa parokia ya Zakhem.
@kimzo3p
@kimzo3p 3 жыл бұрын
Hongereni sana wanacapuchini kwa kazi nzuri mnayofanya kiimani na maendeleo..am blessed
@paulinaluambano9150
@paulinaluambano9150 3 жыл бұрын
Hongereni sana waamini wa parokia ya Zakhem. Hakika kanisani na mazingira kwa ujumla yanapendwza na kuvutia kwa ibada.Parokia ya ujana wangu.😍
@dicksonntaukenga1108
@dicksonntaukenga1108 Жыл бұрын
Asante Sana wazee wanasema
@amaniabel9487
@amaniabel9487 3 жыл бұрын
Utume wako unaprosper sana mungu aendelee kukusindikiza ndg kessy
@mamybaby8790
@mamybaby8790 4 жыл бұрын
Mungu akutunze uendelee kuitenda kaz yake mungu
@raykanyama4463
@raykanyama4463 Жыл бұрын
hongera sanaaaaaa baba
@bridgeterpilla2773
@bridgeterpilla2773 3 жыл бұрын
God bless you Baba Mungu aendelee kukusimamia
@leocadiabwire512
@leocadiabwire512 Жыл бұрын
Hongera baba
@theodoratungaraza2214
@theodoratungaraza2214 2 жыл бұрын
Hongera father kessy
@billgussy6099
@billgussy6099 2 жыл бұрын
Hongera kwa huduma baba
@lucasmasasi5409
@lucasmasasi5409 4 жыл бұрын
Kazi njema kabisa Ndugu.
@maprosokelly2986
@maprosokelly2986 Жыл бұрын
Hakika kunavutia hongera san paroko
@consolataantony7365
@consolataantony7365 4 жыл бұрын
asante mopia
@mary-stellakivali8872
@mary-stellakivali8872 3 жыл бұрын
Hongereni sana
@sylvestrengwelu2012
@sylvestrengwelu2012 3 жыл бұрын
Hongera BABA
@ThinkMedia01
@ThinkMedia01 3 жыл бұрын
Kazi njema kabisa. Huu ni mfano wa kuigwa
@florahmsuya8412
@florahmsuya8412 Жыл бұрын
😂Hela za kanisa ukiziiba hazina baraka yani huyu father nampenda sana Mtani wangu huyu anachekesha
@ladislausblacy9951
@ladislausblacy9951 4 жыл бұрын
Very nice, keep up the good work!
@denisimasunzu729
@denisimasunzu729 3 жыл бұрын
Baba nimependa hayo mazingira hususa nihiyo simlizi waumini na uaminifu ukitumia vizuri fedha ya parokia utabarikiwa bila kujijua mh.....
@deokessy6596
@deokessy6596 2 жыл бұрын
High intelligent quantity
@bahatiagape7121
@bahatiagape7121 2 жыл бұрын
Fr prosper naomba no yako.na shida na wewe
@theodoratungaraza2214
@theodoratungaraza2214 2 жыл бұрын
Pazuri
@ceciliamlamtulu9123
@ceciliamlamtulu9123 2 жыл бұрын
Good job paroko na wana parokia
@kanyeshahigirimana5686
@kanyeshahigirimana5686 Жыл бұрын
sanaa
هذه الحلوى قد تقتلني 😱🍬
00:22
Cool Tool SHORTS Arabic
Рет қаралды 36 МЛН
Fortunately, Ultraman protects me  #shorts #ultraman #ultramantiga #liveaction
00:10
Bony Just Wants To Take A Shower #animation
00:10
GREEN MAX
Рет қаралды 7 МЛН
KUBETI  MKOJANI/NAGWA
17:06
OSO ONLINE TV
Рет қаралды 404 М.
MAPOKEZI YA PAROKO MPYA  PAROKIA YA KIGOMA PADRI FIDELIS BWOYA
16:44
KATOLIKI KIGOMA Online TV
Рет қаралды 2,9 М.
KULA 'APPLE' BAADA YA NUSU SAA- PROF. JANABI
2:47
Daily News Digital
Рет қаралды 14 М.
Niache Niende
7:01
SWAHILI CATHOLIC SONGS
Рет қаралды 482 М.