Рет қаралды 3,650
Mahitaji
Wali vikombe 2
Maji vikombe 2
Chumvi kijiko Cha chai 1
Mafuta kijiko 1 na nusu Cha chakula
Butter ( sio lazima)
Matayarisho
1: Pima vikombe viwili vya mchele. Weka kwenye chombo.
2: Washa jiko, bandika maji jikoni acha yachemke kabisa.
3: Osha Michele ( usiloweke kabisa). Osha kawaida Kutoka starch na uchafu uliopo kwenye mchele.
4: Maji yakishachemka weka chumvi na mafuta. Koroga vizuri. Onja kama chumvi imetosha.
5: Mimina mchele kwenye Maji yaliyopo jikoni. Funika vizuri. Hakikisha mfuniko inatosha vizuri kwenye surufia na mvuke hautoki. Kama mfuniko hautoshi. Funika na foil paper kisha funika na mfuniko juu .
6: Punguza moto acha wali uive taratibu kwa moto mdogo sana. Usigeuze wali.
7: Kama unapenda wali utoke vizuri mmoja mmoja , epuka kugeuza. Hakikisha Maji yamekauka kabisa. Hakuna hâta tone ndio uguze.
8: Ukishaugeuza, kama wali bado una kiini usiongeze maji. Funika vizuri uache. Unapofunika mvuke unaotoka kwenye wali, unapokutana na mfuniko juu au foil unageuka kua maji.
9: Mvuke huo ndio utaivisha chakula. Acha Dakika 5 Kisha epua chakula chako kitakua tayari.
8: Jirambe!
Tips za kutoa wali mmoj mmoja
1.Ujue mchele wako wahitaji maji kiasi gani. kila mchele unakunywa maji kivyake.
2.Jaribu kutokoroga at least zaidi ya mara mbili.
3.Usitumie moto mwingi kufiinikia kama unatumia jiko la mkaa.