Рет қаралды 27,831
Saa chache mara baada ya Watanzania kupokea taarifa njema naya Baraka kutoka Vatican kwa Papa Fransis ya uteuzi wa Askofu Mwandamizi Protase Rugambwa kuwa Kadinali wa Kanisa Katoliki Nchini Tanzania kupitia ardhi ya mkoa wa Tabora, Mkuu wa Mkoa huu Balozi batilda salha Burian anafika katika ofisi za Kadinali zilizopo Kanisa Katoliki Jimbo kuu tabora kwa lengo la kuwasilisha salumu za Pongezi kutoka kwa Mheshimiwa Rais, Daktari Samia Suluhu Hassan.
Kadinali Rugambwa kwa unyenyekevu mkubwa amepokea salamu hizi za Mheshimiwa Rais zilizoletwa kwake kwa niaba na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mheshimiwa Balozi Daktari Batilda Salha Burian,
Kupitia uteuzi huu uliofanywa Jumapili Julai 9, 2023, Kadianali Protase Rugambwa anakuwa Kadinali wa tatu (03) Nchini Tanzania akitanguliwa na Kadinali Laurean Rugambwa aliyefariki dunia Disemba 9, mwaka 1997 na kisha Kadinali Polycarp Pengo aliyestaafu mwaka 2019.
Uteuzi huu uliofanywa na Papa Fransis unaoendelea kuandika historia njema kwa Nchi ya Tanzania, umekuja ikiwa ni takribani miezi mitatu tangu alipomteua Kadinali Rugambwa kuwa askofu Mwandamizi Jimbo Kuu Katoliki Tabora.
Kwa habari na Matukio yote Muhimu yenye Maslahi mapana kwa UMMA, wasiliana nasi kwa +255 764 736 372, +255 787 721 965 Barua pepe, toronto21onlinetv@gmail.com, Tufuatilie katika Mitandao yetu ya Kijamii, KZfaq, Twitter, Facebook na Instagram kwa jina la Torontotv Tabora. "Toronto Online Tv - habari na matukio tumekufikia"