Рет қаралды 6,015
Muuguzi wa afya katika Hospitali ya KCMC, Lenga Masunga Ng'hajabu anadaiwa kupotea katika mazingira ya kutatanisha baada ya kutoonekana kazini kwa siku 5 huku simu zake za mkononi zikiwa hazipatikani.
Ng'hajabu ambaye ni Muuguzi katika idara ya masikio, pua na koo katika hospitali hiyo, anadaiwa kutoonekana kazini tangu Julai 4, mwaka huu ambapo mpaka sasa hajulikani alipo.
Mwananchi digital leo ilifika katika hospitali hiyo na kuongea na Ofisa Uhusiano wa hospitali hiyo, Gabriel Chisseo akizungumzia juu ya tukio hilo afisa uhusiano wa hospitali hiyo amesema muuguzi huyo ametoweka tangu tarehe 3 mwezi julai mwaka huu na mpaka sasa hakuna taarifa inayotia matumaini huku simu zake zikiwa hazipatikani.
Mwananchi Digital haikushia hapo ilienda kutembelea makazi yake anapoishi na kuongea na mwenye nyumba, Robert Mwakalinga ambae Ng'ahabu alikuwa anaishi kama mpangaji amesema mara ya mwisho kumuona ni siku ya jumanne na hakutoka lakini asubuhi alikuta mlango upo wazi hali ambayo haikua ya kawaida.