Рет қаралды 1,375
Mfanyabiashara ndogondogo (Machinga), John Gerald (30) anayefanya shughuli zake katika Soko la Sabasaba jijini Dodoma, amekutwa amefariki dunia akidhaniwa kupigwa na kitu kizito kichwani.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Theopista Mallya
leo Julai 12, 2024, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo usiku wa kuamkia Julai 11 mwaka huu, wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma.
Kamanda Mallya amesema kuwa chanzo cha mauaji hayo ni ugomvi uliozuka katika klabu ya pombe ya kienyeji katika eneo la Mnada Mpya, ambapo marehemu alikuwa na marafiki zake ambao hawakufahamika na juhudi za kuwatafuta zinaendelea. (Imeandaliwa na Hamis Mnha)