Рет қаралды 1,284
Maziwa ya soya ni kinywaji kinachofanana na maziwa lakini kinatokana na mbegu za soya .Maziwa ya soya asili yake ni huko Nchini China ambapo soya imetokea.na Baadaye, mimea ya soya na vyakula vyake vilikuja Japan na mpaka kusambaa Duniani kote.
Hata hivyo ni zao mojawapo katika mazao ya jamii ya mikunde ambalo Kwa Nchi yetu ya Tanzania hulimwa kwa wingi katika mikoa ya Mtwara, Ruvuma, Morogoro, Rukwa, Lindi, Mbeya, Iringa na Arusha.
Zao hili huwa na virutubisho vingi kama vile wanga, protini, mafuta, madini na hata vitamini. Aidha, lina sifa ya kuwa na kiasi kikubwa cha protini kinachofikia hadi asilimia 40.
Soya ni zao la muda mfupi ambalo hukomaa ndani ya miezi mitatu hadi mitano toka kupandwa kulingana na aina, na pia hata hali ya hewa na mwinuko kutoka usawa wa bahari.