Рет қаралды 7,239
Moshi. Wakati wananchi wanaoishi kijiji cha Kiraracha Marangu wilaya ya Moshi wakimwelezea Augustine Mrema kama alikuwa mtu mwema na mkarimu, nyumbani kwake hadi leo Agosti 21,2022 hapakuwa na harakati kubwa za msiba wake.
Hii ni kwa sababu Mrema aliyekuwa mwenyekiti wa Tanzania Labour Party (TLP) na Mbunge wa Vunjo, kuwa na makazi mengine Jijini Dar es Salaam ambako alifariki dunia akitibiwa hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) leo asubuhi.
Wakizungumza na Mwananchi Digital katika kijiji hicho cha Kiraracha baada ya kupokea taarifa za msiba huo, majirani zake walimwelezea kama mtu mwema, mkarimu na anayependa kusaidia majirani bila kujali itikadi za kisiasa, kiuchumi, jinsia au umri.