Рет қаралды 573
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Watanzania wana kila sababu ya kutembea kifua mbele na kujivunia utafiti uliofanyika hapa nchini na kupata mbegu mpya ya michikichi ambayo imeonesha mafanikio makubwa.
“Baada ya kukaa na kufanya tathmini ya zao la chikichi hapa Tanzania, na leo nimesikia michango ya wadau wote. Nimejiridhisha kwamba utafiti tulioufanya wa kuzalisha mbegu ya Tanzania ambayo inaota na kutoa matunda ndani ya miaka miwili hadi mitatu, ninayo furaha kutamka kuwa utafiti ule umefanikiwa,” alisema na kuamsha shangwe miongoni mwa wadau wa zao hilo.
Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo wakati akihitimisha kikao chake na wadau wa zao la chikichi mkoani Kigoma kwenye ukumbi wa NSSF. Mbegu hiyo bora ya michikichi aina ya TENERA inatoa mafuta mara tatu zaidi ya aina ya DURA ambayo inalimwa na wakulima kwa takribani asilimia 90.
Alisema mtu yeyote anayetaka kulima chikichi anaweza kufanya hivyo kwa sababu mbegu zipo. “Tulianza kuzalisha mbegu mwaka 2018 na ilipofika mwaka 2020 tukaanza kupanda miche na leo tunaona matunda yanapatikana.”
Follow us on:
FACEBOOK;
SpotiLeo: / spotileo-176. .
HabariLeo: / habarileo
DailyNews: / dailynewstz
INSTAGRAM;
HabariLeo: habarileo_tz?ig...
SpotiLeo: spotileo?igshid...
TWITTER;
Twitter HabariLeo: HabariLeo?s=09