Рет қаралды 642
Hii ni sehemu ya kwanza ya mazungumzo maalum kati ya The Chanzo na Idris Sultan ambapo msanii huyo anazungumzia kwa upana tasnia ya filamu na sanaa ya ucheshi nchini Tanzania.
Sultan, ambaye pia anaigiza, anasema kwamba kuna mambo yanapaswa kurekebishwa Tanzania ili tasnia ya filamu iweze kutimiza lengo lake vizuri kwenye jamii.
Moja ya mambo anayofikiria yanapaswa kufanyika ni mamlaka husika kuruhusu utungwaji wa filamu kulingana na umri wa mtumiaji, uamuzi utakaondosha utaratibu wa sasa ambapo filamu zote zinazotengenezwa ni lazima ziweze kuangaliwa na watoto.
Sultan anaamini kwamba sharti hili linadumaza ubunifu wa wanafilamu, na anatoa wito kwa mamlaka husika kufanya mageuzi kwenye eneo hilo.
Unaweza kutufuatilia kupitia;
TWITTER: / thechanzo
INSTAGRAM: / thechanzo
FACEBOOK: / thechanzo
TIKTOK: www.tiktok.com....
Au tembelea tovuti yetu: www.thechanzo.com
Je, una habari? wasiliana nasi kupitia Telegram/WhatsApp +255 753 815 105
The Chanzo Initiative, 2024 © All Rights Reserved.