Рет қаралды 386
Wiki hii Bongo5TV ilikutana na msichana, Sophia ambaye ameanza kubobea kwenye uinjinia wa umeme ambapo kwa sasa tayari ameanza kutengeneza baadhi ya vifaa ambavyo mara nyingi vilikuwa vinaagizwa nje ya nchi.
Sophia ambaye kwa sasa yupo Sido, Vingunguti amesema anaipenda sana kazi hiyo licha ya kukutana na changamoto za baadhi ya watu kutowaamini wanawake ambao wanafanya kazi za aina hiyo kwa madai wanaonekana hawawezi kuhimili mikiki mikiki.