Рет қаралды 26,031
Je, mtazamaji unajua kuna nyama isiyotoka kwenye mifugo na ambayo hutengenezwa kwa kutumia mimea? Na je unajua kuna teknolojia inayotumia mawimbi ya sauti inayosababisha vifaranga wa kiume wakiwa ndani ya mayai kubadilika na kuwa kuku ili kutaga mayai? Hizo ni baadhi ya uvumbuzi wa wataalam nchini Israeli ambao wanalenga kubadilisha jinsi sekta ya kilimo itakavyokuwa katika miaka ya baadaye. Mwanahabari wetu Gatete Njoroge alizuru taifa hilo na kutuandalia taarifa ifuatayo kuhusu kilimo mambo leo.