Рет қаралды 5,199
Watu watatu wamefariki dunia wakiwemo mapadri wawili na wengine wawili kujeruhiwa baada ya gari walilokuwa wamepanda kupata ajali katika eneo la Mtama mkoani Lindi.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi ACP, John Imori akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake leo Ijumaa Julai12, 2024 amesema kuwa ajali hiyo imetokea saa12.00 asubuhi katika eneo la Mtualonga Barabara ya Masasi -Mnazi Mmoja katika Halmashauri ya Mtamaa mkoani Lindi.
Amesema gari aina ya Mitsubishi Outlander iliyokuwa ikitokea Ndanda kuelekea jijini Dar es Salam ililipiga shimo na kupoteza mwelekeo na kuacha njia kisha kutumbukia kwenye shimo la karavati na kusababisha vifo na majeruhi wawili.
Kamanda Imori amewataja waliofariki kuwa ni Cornelius Modoe (55), Padri wa Kanisa Katoliki wa jijini Dar es Salaam, Pius Boa (51) na Padri wa Kanisa Katoliki na mkazi wa Tanga Haphymark Mkenda (51).
Imeandikwa na Bahati Mwatesa