UTUNZAJI SHAMBA LA MIGOMBA-MAMBO TISA MUHIMU-SURA YA SITA (SEHEMU YA TATU) 5.KUONDOA UA LA KIUME Ndizi ina sehemu ya kike /maua ya kike ambayo hukua na kuwa matunda ya kula na ua la kiume. Ni muhimu kuondoa ua la kiume mara moja pindi maua ya kike yanapoanza kunyooka na kuelekea juu. Kuliacha ua la kiume ni kuyafanya matunda yawe madogo kwa kushindania chakula na ua la kiume. Pia uwepo wa ua la kiume huvutia nyuki ambao huja kufyonza nekta (Ute mtamu) kwenye ua la kiume na hivyo kuweza kueneza magonjwa ya fangasi,virusi na bacteria kwenye shamba zima.Ua la kiume inashauriwa liondolewe ndani ya kipindi cha wiki mbili tangu mkungu uchanue kutoka kwenye shina la mgomba. Uodoaji ufanyike kwa kutumia vifaa visivyo na ncha kali ;mfano mti mrefu wenye pacha badala ya kutumia panga.Migomba yote ikaguliwe mara kwa mara ili kuhakikisha haina ua la kiume linaloning'inia. 6.MITI YA KUIKINGA WENYE NDIZI USIANGUKE Zoezi la kuweka miti ya kukinga migomba isianguke lianze mara tu mikungu inavyoanza kutokea. Ni dhahiri uwepo wa mkungu kwenye shina la mgomba huongeza uzito na kupelekea mgomba kuanguka kwa urahisi hasa kipindi cha upepo mkali. Ni muhimu kutumia miti imara inayoweza kuhimili uzito wa shina na mkunga katika vipindi vya upepo mkali. 7.KUONDOA MAJANI MAKUUKUU Kuondoa majani makuukuu kwenye migomba husaidia kupunguza uwekezekano wa kujificha wadudu na wanyama hatari kwenye shamba la migomba. Pia majani haya hutumika kama matandazo. Majani yote yaliyokauka na kuning'inia yakatwe na kutandazwa chini. Uwepo wa majani haya ni hatari kwa sababu pia huzuia mzunguko mzuri wa hewa na husababisha kuenea kwa urahisi wa magonjwa shambani.Ni muhimu SHAMBA liwe safi lenye mzunguko mzuri wa hewa na uoto wa kutosha. Endelea kujifunza.. SUBSCRIBE HAPA :www.youtube.com/@aje-farmsmashambayanayotem7392 Uliza SWALI kwenye comment 👇 Agiza kitabu na uunganishwe kwenye group ya WhatsApp BURE.WhatsApp 0757757968 ili kuagiza kitabu. #ajefarms #mashambayanayotembea #MIGOMBA #kilimo #LikeAndShare #Subscribe #youtubers
@aje-farmsmashambayanayotem73927 ай бұрын
UTUNZAJI SHAMBA LA MIGOMBA - MAMBO MUHIMU TISA YA KUZINGATIA -SURA YA SITA (SEHEMU YA KWANZA) UTUNZAJI WA SHAMBA LA PASHENI -MAMBO MUHIMU 6 YA KUZINGATIA -SURA YA 4 (SEHEMU YA KWANZA) Utunzaji wa shamba la migomba ni pamoja na PALIZI,KUWEKA MATANDAZO,KUONDOLEA MACHIPUKIZI YA ZIADA,KURUTUBISHA SHAMBA,KUONDOLEA SEHEMU ZA MAUA YA KIUME,KUWEKA KINGA ZA MITI NDIZI ZISIANGUKE, KUPUNGUZA MAJANI MAKUUKUU PAMOJA NA ULINZI NA UVUNAJI NDIZI.Kila kazi ina masharti na miiko yake - mtaka cha uvunguni sharti ainame ! Ili kupata mavuno bora lazima ufuate masharti na miiko hii. Hamna mkato. Kila hatua ina gharama ,kanuni,masharti na bajeti zake .Soma hadi mwisho ili ujifunze mambo muhimu tisa ya kuzingatia kwa kila hatua ukihitaji kulima kilimo cha migomba kibiashara. 1.PALIZI: Bila palizi za wakati mavuno yatakosekana au yanaweza kuwa hafifu kabisa. Magugu kwenye shamba la migomba yana hasara nyingi bila faida - mosi hushindana na mimea ya migomba kupata chakula,pili huleta magonjwa shambani na tatu huweza kuficha adui na wanyama hatari kama panya na nyoka. Ili kupata MAFANIKIO hakikisha unafanya palizi kila wakati kila yatakapotekea. Kwenye mikoa yenye mvua nyingi palizi ni kila baada ya miezi 2 hadi mitatu. Fanya palizi kabla ya magugu kutoa mbegu ili kuepusha mbegu za magugu zisisambae na kuota tena na hivyo kufanya gharama ya palizi kuwa kubwa.Unaweza kutumia jembe la mkono lenye meno kwa kutifua kuepuka kuharibu mizizi au kwa kutumia mikono kwa shamba dogo na kama una vibarua wa kutosha au la ni rahisi na nafuu kutumia dawa za kuua magugu kwa mashamba makubwa kwa utaratibu utakaoelekezwa na muuza dawa hizo. Ni muhimu kutumia dawa sahihi na kwa umakini shambani kwa afya yako,mimea na hata mtumiaji wa matunda utakayovuna.Palizi huanza mara tu baada ya miche kupandwa shambani ,usiruhusu gugu shambani! Ndio siri ya MAFANIKIO. 2.MATANDAZO :Ili kupunguza gharama za palizi ni muhimu kuweka matandazo na unaweza kujifunza zaidi kuhusu matandazo kupitia AJE-FARMS MASHAMBA YANAYOTEMBEA huko KZfaq. Matandazo yana faida nyingi ikiwemo : kuzuia magugu yasiote, kurutubisha shamba yakioza,kuzuia mmonyoko wa udongo, kupunguza upotevu wa madini muhimu/virutubisho kwenye udongo kwenye maeneo yenye mvua nyingi kwa udongo kuoshwa na mvua nyingi (leaching), kupunguza joto la udongo na muhimu zaidi kutunza unyevunyevu shambani hasa kwa mikoa yenye ukame.Matandazo ni mabaki ya mimea ikiwemo mpunga,makapi ya kahawa,majani ya migomba,nyasi za porini,mabua ya mahindi nk. Ni nafuu sana na yanapatikana kwa wepesi. Kwa maeneo ambayo hayapatikani yanaweza kutumika matandazo ya plastiki (plastick mulching) ambayo si bora kama yalivyo matandazo ya mabaki ya mimea kwani plastiki haiozi kuwa mbolea. Wakati wa kutandaza matandazo acha umbali wa sm 10 hadi 20 kutoka kwenye shina la mmea (duara ya wazi kuzunguka shina la mmea) ili kuepuka uwezekano wa shina kushambuliwa na magonjwa kupitia wadudu kama mchwa au sisimizi. Je,una swali ? Uliza kwenye comment section na utajibiwa mara moja.Somo hili linaendelea... Ili kujifunza zaidi kwa vitendo SUBSCRIBE hapa www.youtube.com/@aje-farmsmashambayanayotem7392 Weka oda yako ya KITABU CHA KILIMO CHA MIGOMBA/ PASHENI /CHIKICHI -WhatsApp 0757757968 -Gharama ya kitabu Soft copy ni TZS 5,000 na hard copy ni TZS 10,000 na kila atakayenunua kitabu ataunganishwa kwenye group ya WhatsApp BURE. #ajefarms #mashambayanayotembea #kilimo #Subscribe #MIGOMBA #masoko #LikeAndShare
@severngama1217 Жыл бұрын
Miche mnauza sh ngapi?
@aje-farmsmashambayanayotem7392 Жыл бұрын
Miche ya kwenye mifuko ni kati ya 2500/= hadi 5000/= na vikonya ni kati ya 1000/= hadi 2500/= Kwa maelezo zaidi tupigie :- 0757757968
@aje-farmsmashambayanayotem73927 ай бұрын
UTUNZAJI SHAMBA LA MIGOMBA-MAMBO TISA MUHIMU-SURA YA SITA (SEHEMU YA TATU) 5.KUONDOA UA LA KIUME Ndizi ina sehemu ya kike /maua ya kike ambayo hukua na kuwa matunda ya kula na ua la kiume. Ni muhimu kuondoa ua la kiume mara moja pindi maua ya kike yanapoanza kunyooka na kuelekea juu. Kuliacha ua la kiume ni kuyafanya matunda yawe madogo kwa kushindania chakula na ua la kiume. Pia uwepo wa ua la kiume huvutia nyuki ambao huja kufyonza nekta (Ute mtamu) kwenye ua la kiume na hivyo kuweza kueneza magonjwa ya fangasi,virusi na bacteria kwenye shamba zima.Ua la kiume inashauriwa liondolewe ndani ya kipindi cha wiki mbili tangu mkungu uchanue kutoka kwenye shina la mgomba. Uodoaji ufanyike kwa kutumia vifaa visivyo na ncha kali ;mfano mti mrefu wenye pacha badala ya kutumia panga.Migomba yote ikaguliwe mara kwa mara ili kuhakikisha haina ua la kiume linaloning'inia. 6.MITI YA KUIKINGA WENYE NDIZI USIANGUKE Zoezi la kuweka miti ya kukinga migomba isianguke lianze mara tu mikungu inavyoanza kutokea. Ni dhahiri uwepo wa mkungu kwenye shina la mgomba huongeza uzito na kupelekea mgomba kuanguka kwa urahisi hasa kipindi cha upepo mkali. Ni muhimu kutumia miti imara inayoweza kuhimili uzito wa shina na mkunga katika vipindi vya upepo mkali. 7.KUONDOA MAJANI MAKUUKUU Kuondoa majani makuukuu kwenye migomba husaidia kupunguza uwekezekano wa kujificha wadudu na wanyama hatari kwenye shamba la migomba. Pia majani haya hutumika kama matandazo. Majani yote yaliyokauka na kuning'inia yakatwe na kutandazwa chini. Uwepo wa majani haya ni hatari kwa sababu pia huzuia mzunguko mzuri wa hewa na husababisha kuenea kwa urahisi wa magonjwa shambani.Ni muhimu SHAMBA liwe safi lenye mzunguko mzuri wa hewa na uoto wa kutosha. Endelea kujifunza.. SUBSCRIBE HAPA :www.youtube.com/@aje-farmsmashambayanayotem7392 Uliza SWALI kwenye comment 👇 Agiza kitabu na uunganishwe kwenye group ya WhatsApp BURE.WhatsApp 0757757968 ili kuagiza kitabu. #ajefarms #mashambayanayotembea #MIGOMBA #kilimo #LikeAndShare #Subscribe #youtubers