Рет қаралды 976
T.Maelekezo ya Waziri Mkuu uchaguzi wa Serikali za mitaa
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameielekeza Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) kushirikiana na wadau mbalimbali kufanikisha maandalizi ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika baadaye mwaka huu.
Majaliwa ametoa maelezo wakati akitoa hoja ya kuahirisha mkutano wa 14 wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ieo Ijumaa, Februari 16, 2024.
Aidha Majaliwa amewataka wasimamizi wa maboresho ya daftari la kudumu la wapiga kura kutoa elimu ya mpiga kura kwa makundi yote, kuwafikia Wananchi wote na kuwawezesha kuelewa sheria, kanuni na taratibu za mchakato mzima wa uchaguzi.