Рет қаралды 16,296
Askofu wa KKKT, Dayosisi ya Mashariki na Pwani, Dk Alex Malasusa leo Jumapili ametangaza msamaha kwa Mchungaji wa Ushirika wa Kijitonyama, Dk Eliona Kimaro ambaye alipewa likizo ya siku 60.
Usiku wa Januari 16, 2023 ilisambaa video ikimuonyesha mchungaji Kimaro akiwaeleza waumini wake kuwa amepewa likizo ya siku 60 baada ya kuitwa katika ofisi ya msaidizi wa askofu na kufanya kikao na mkuu wa jimbo.
Lilizo hiyo ilikuwa inamalizika Machi 17, 2023 na Mchungaji Kimaro alipokuwa akiwaaga Washirika wa Kijitonyama alisema baada ya likizo hiyo hatarudi hapo, alielezwa akaripoti Makao Makuu ya Dayosisi.
Katika msamaha huo wa leo, umetangazwa katika Ibada iliyofanyika Ushirika wa Kinyerezi, Tabata na kuongozwa na Askofu Malasusa ambapo ametangaza uamuzi huo Kanisani baada ya Mchungaji Kimaro kupewa fursa ya kuwasalimia waumini na akaomba radhi kwa yote yaliyotokea.