Рет қаралды 15,286
Vazi hubeba utambulisho wa mtu. Kama ambavyo kupitia vazi la mtu unaweza kujua mtu ni nani, vilevile vazi hubeba utambulisho wa mtu kiroho. Kuna vazi ukivalishwa basi kuna aina za roho za giza zitakufuatilia.Kwa mfano ukivishwa vazi la kukataliwa basi roho za kutoonekana,roho za mauti, umasikini no zitakufuatilia tu.
Katika vita hii ya Mfalme wa Shamu na Israeli,jeshi la Shamu lilipewa maelekezo kuwa wasimuue yeyote bali yule mwenye mavazi ya kifalme,mauti ilikuwa ndani ya vazi na ndio maana Yehoshafati(mfalme wa Yuda) alinusurika kuuawa maana yeye ndiye aliyekuwa na mavazi ya kifalme na Mfalme aliyekuwa anatafutwa amevaa mavazi ya kawaida.
Mfalme wa Israeli alikuwa na maarifa juu ya hiyo vita na akajua kabisa kuwa kitakachohusishwa ni vazi ambalo ndilo litakalomtambulisha na hivyo mauti kumfuata. Kuna vazi toka uvalishwe rohoni basi maisha yako yameharibika kabisa, kukemea hiyo changamoto bila kuvua hilo vazi ulilovishwa ni ngumu sana kuona matokeo.
#PastorSunbella#Ufahamu#WaKiMungu