Рет қаралды 21,942
Leo katika Clinic ya ujasiriamali, Prof. Ngowi anatembelea kampuni ya GLOBAL EDUCATION LINK LTD, na kufanya mahojiano na Mkurugenzi wa kampuni hiyo, Bwana Abdulmalik Mollel, ambaye anamweleza Prof. Ngowi kwamba wakati anaanzisha kampuni hiyo hakuwa hata na shilingi moja mfukoni mwake, lakini leo kampuni ya GLOBAL EDUCATION LINK LTD, ni kampuni kubwa na yenye mafanikio si tu Tanzania lakini katika ukanda huu wa Afrika ya mashariki. Nini siri ya mafanikio hayo, Ungana na Prof. Ngowi kwenye kipindi hiki ili nawe ujifunze Kutoka kwa mjasiriamali huyu jinsi ya kukua katika biashara.