Рет қаралды 2,196
Chakula cha kuku wanaoanza kutaga huwa na kiwango muhimu cha Protini (Digestible Crude Protein) kuanzia asilimia 16 . Chakula hicho ni muhimu kikawa na madini ya Calcium (Chakula chenye chokaa) kwa ajili ya utengenezwaji wa magamba ya mayai. Kuku ambao wana kiwango kidogo cha calcium hutumia akiba ya madini haya ya calcium iliyopo kwenye mifupa yao kutengenezea magamba ya mayai. Anza kuwapa kuku chakula hiki wakifikia umri wa kuanzia wiki ya 19