Рет қаралды 485
Rais Samia Suluhu Hassan amemtaka Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk Seleman Jafo kufanya kazi kwa ukaribu na wafanyabiashara wa Kariakoo na kuhakikisha changamoto zote zilizopo zinatatuliwa.
Rais Samia amesema mgomo uliofanyika hivi karibuni alituma watu mbalimbali kuwahoji kwa nini wafanyabiashara hao wanagoma lakini walijibu hawajui kwa nini wanagoma.
"Nilituma watu kwa siri waende Kariakoo wamewauliza watu kwa nini wanagoma wengi wao wanasema sisi hatujui kwa nini tunagoma, tumeambiwa na viongozi fungeni maduka sisi tukafunga, tumeambiwa msiuze hatuuzi lakini kuna nini ndani yake sisi hatujui. Kwa hiyo ukiangalia kwa undani kuna siasa Kariakoo, sasa ili kuondoa hizo siasa nenda ukawasikilize."
Rais Samia amesema hayo leo Julai 5, 2024 wakati akiwaapisha viongozi mbalimbali aliowateua hivi karibuni.