Рет қаралды 208
Mkurugenzi wa huduma za Afya lishe na Ustawi wa Jamii kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Dkt.Rashidi Mfaume Julai 1,2024 wakati wa Ziara ya ukaguzi wa huduma za Afya katika Halmashauri ya Mji Njombe ,ametoa pongezi kwa hospitali ya Mji wa Njombe(Kibena) kwa kuwa na kitengo cha mfano cha kuhudumia watoto wanaozaliwa na uzito pungufu (Njiti) pamoja na usimamizi mzuri wa usafi wa mazingira uliowezesha hospitali hiyo kushika nafasi ya pili kwenye tuzo za usafi wa mazingira mwaka 2023.