Рет қаралды 275
Mungu ni mkubwa kuliko sisi na tusitarajie kumuelewa katika kila jambo. Utatu ni jambo gumu kulieleza kwa kina. Hakuna mwanadamu anayeweza kulielewa kwa undani zaidi. Biblia inafundisha kuwa Baba ni Mungu, ya kuwa Yesu ni Mungu na pia Roho mtakatifu ni Mungu. Biblia pia inafundisha kuna Mungu mmoja tu. Ijapokuwa tunaweza kufahamu uhusiano tofauti tofauti wa sehemu za utatu huu ni vigumu kuelewa kwa akili ya kibinadamu. Hii haimaanishi kuwa si kweli au si maagizo ya Biblia.