Рет қаралды 4,663
Katika mfululizo wa makala kuhusu vijana walio chini ya miaka 30 mbapo huangazia vijana waliofanya vizuri na wanaoendelea kufanya vizuri katika teknolojia, siasa na kijamii kwa nchi za Afrika Mashariki.
Leo tunae Wadh-Hat Mustafa alianza kujihusha na ujasiriamali akiwa na miaka 23 tu baada ya kuanza kutengeneza manukato yatokanayo na viungo mbalimbali kutoka Zanzibar.
Alianza na Udi baada ya kubaini kuna upungufu wa harufu tofauti tofauti na za kipekee katika marashi hayo.
Anasema wakati wengne wakichukulia biashara ya udi kama ni ya Kimaskini sana yeye aliona fursa ambapo kwa sasa akiwa na miaka 28 anamiliki biashara ya Marashi ya Zanzibar akitengenza manukato mbalimbali aanayosafirisha na kuuza hadi nchi za nje.
Je amewezaji kufika hadi hapo?
Mwandishi wa BBC Veronica Mapunda ametuandalia Habari hii
Video: @marashizanzibar & @frankmavura
#bbcswahili #marashi #ujasiriamali