Рет қаралды 4,336
Watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi Wamevamia na kumuua Faraja Luoga na kisha kumjeruhi Golden Luoga ambaye ni wakala wa fedha mjini njombe kwa kuwapiga risasi sehemu mbalimbali za mwili baada ya kuvamiwa nyumbani kwa goldeni luoga mtaa wa Kambarage eneo la Galuhenga.
Tukio hilo limetokea augusti 29 majira ya saa tatu usiku ambapo kwa mujibu wa majirani wamesema walisikia milio miwili ya risasi ikitokea nyumbani kwa jirani.
Mwenyekiti wa mtaa wa Kambarage France Msanga alisema kuwa alipigiwa simu majira ya saa tatu na dakika 20 usiku ndipo alipofika eneo la tukio.
Naye makamu mwenyekiti wa mawakala mkoa wa Njombe Rehema Mabuga alisema tukio hilo sio la kwanza kutokea ni kama tukio la sita.