Рет қаралды 2,379
Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi Jerry Silaa amekitaka chama cha mapinduzi ccm kuwafukuza pamoja na kuwachukulia hatua kali wenyeviti vijiji,vitingoji na wa mitaa ambao wamewaingiza wananchi kwenye migogoro ya Ardhi.
Silaa ameyasema hayo mbele ya Amos Makala katibu mwenezi Taifa kwenye mkutano wa hadhara wa chama cha mapinduzi wenye lengo la kusikiliza kero za wananchi katika jimbo la Ukonga jijini Dar Es Salaam.