Рет қаралды 12,181
Familia moja eneo la Kangemi, Nairobi inalilia haki baada ya jamaa yao kufariki katika njia tata wakati wa maandamano ya wiki iliyopita. Familia ya wycliffe kane aliyekuwa mhudumu wa boda boda inasema jamaa yao aligongwa na kifaa butu huku kukiwa na madai kuwa huenda aligongwa na kitoa machozi kabla ya kupoteza mwelekeo na kuanguka na pikipiki.