Рет қаралды 4,981
Akofu wa Kanisa Katoliki jimbo la Geita Dk Flavian Kassala amesema kama kanisa wanatia shaka taarifa iliyotolewa na jeshi la polisi kuwa kijana Elpidius Edward (22) alikuwa mlevi na kuliomba jeshi hilo kufanya uchunguzi wa kina kwa kuwa matendo aliyoyatenda yalitendeka kimkakati na mtuhumiwa alimaanisha
Akitoa salamu za shukrani wakati wa ibada ya kutakatifuza kanisa hilo iliyoongozwa na Askofu mstaafu wa kanisa Katoliki jimbo kuu la Dar es Salaam Kadinali Polycarp Pengo,Askofu Kassala ameliomba jeshi la polisi kuchunguza kwa kina tukio hilo lililosababisha maumivu kwa kanisa.