Рет қаралды 3,543
Uandaaji wa mashimo.
Miche ya miti ya matunda kama machungwa, migomba, na milimau hupandwa kwa nafasi ya mita 5 hadi 7 kati ya mche na mche, mita 6 hadi 8 kati ya mstari na mstari, shimo linatakiwa kuwa na upana na kina cha futi 2 hadi 3, kutegemeana na hali ya udongo wakati wa kuchimba shimo udongo wa juu ulio na rutuba na ule wa chini usio na rutuba ni lazima utenganishwe.
Udongo wa juu ulio na rutuba unaweza kuweka kulia kwako na ule usio na rutuba unaweza kuweka kushoto kwako. Hakikisha samadi (iwe imetokana na ile ya ng`ombe, mbuzi au kuku) iliyo iva vizuri au yenye iliyopoa vyema, changanya samadi na ule udongo wa juu ulio weka kulia kwako kisha jaza mchanganyiko huo ndani ya shimo, Shimo lazima lijazwe udongo hadi kutengeneza mwinuko wenye kitako cha sm 50 - 100 na kimo cha sentimeta 10 toka usawa wa ardhi