Рет қаралды 1,148
NJOMBE
Wakati Tanzania Leo Ikiungana na Mataifa Mengine Kuadhimisha Siku ya Wabunifu na Wavumbuzi Duniani Baadhi ya Wabunifu Mkoani Njombe Wamesema Wanaamini Maono ya Aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano Hayati Dokta John Magufuli Yataendelezwa Kwa Kuendelea Kuwaunga Mkono.
Wanasema Wanaamini Ubunifu Ndio Unaosaidia Kuongeza Tija Kazini na Kwamba Mataifa Mengi Yaliyoendelea Yalifanikiwa Kwa Kuwaendeleza Wabunifu na Wavumbuzi wa Vitu Mbalimbali Kwa Kuwa Wamekuwa na Mchango Mkubwa Katika Uchumi na Utoaji Ajira.
Kituo Hiki Kimetembelea Chanzo Cha Maji Cha Mbunifu Ruben Mtitu Ali maarifu Kama Kisangani Kilichopo Mkiu Wilayani Ludewa Ambaye Ameanza Kubuni Mradi wa Kuzalisha Umeme wa Kilowati 100 Utakaoendesha Mitambo Yake ya Kuyeyusha Chuma ambaye Anasema ni Lazima Akamilishe Ndoto Yake Hiyo.