Рет қаралды 157,598
Mwaka 1907 inasemekana palionekana tundu kubwa na kipande cha sanda kwenye kaburi alilozikwa Mzee aliyefahamika kwa jina la Mzee Limbende kwenye kijiji cha Nanguruwe kata ya Nanguruwe mkoani Mtwara ambaye alikuwa mmoja wa wazee wa kijiji hicho.
Siku chache baadae Ndugu wa karibu wa Marehemu Mzee Limbende aitwae Salum Binali Walivenga alioteshwa ndoto kwamba Marehem Limbende amefufuka na kuwa nyoka ambae atalinda kijiji hicho na hii ni kimila na desturi.
Tumefika kwenye kijiji hicho na kutembelea kwenye eneo la bwawa kubwa lililopo kijijini hapo ambapo inasemekana kwamba ndio anapoishi nyoka huyo tangu miaka hiyo ambapo anaonekana na Mtu mmoja tu ambaye anatakiwa kupokea maono ya yanayoweza kutokea siku za mbeleni kwa kuoteshwa.