Рет қаралды 148,029
MZUNGUKO wa hedhi, siku salama, siku za uzazi na siku hatari.
mada tutakayozunguka nayo kila Jumanne, kwa siku 15 kaa mkao, kujifunza, mana nimegunduwa wanawake wengi wanapigwa chenga na kalenda na hujikuta haelewi. KWA UTANGULIZI👇👇
ILI UELEWE VIZURI MADA HII MPAKA MWISHO - BASI HUNA BUDI KUJIFUNZA MAMBO KADHAA MUHUMI
Kama wewe ni mara yako ya kwanza kabisa kujifunza mzunguko wa hedhi basi itakufaa kuwa na KALENDA yako ya ukutani na PENI nyekundu na nyeusi kama utaweza.
1- Siku ya kwanza umepata bleed (wengi husema nimeingia siku zangu) ndio siku ya kwanza ya mzunguko wako wa hedhi katika mwezi husika.
2- Siku ya mwisho ya mzunguko wako wa hedhi ni siku moja kabla hujapata hedhi ya mwezi mwingine.
3- Mzunguko wa hedhi sio lazima kila mwezi uje siku ile ile na tarehe ile ile
4- Mzunguko wa hedhi sio lazima kila mwezi uwe na urefu/ukubwa ule ule.
5- Mzunguko wa hedhi ni nini?
Ni idadi ya siku unazochukua kuanzia siku ya kwanza umepata hedhi/bleed mpaka siku moja kabla ya kupata hedhi ingine ya mwezi mwingine.
6- Siku za Hedhi ni nini?
Siku za Hedhi ni siku kuanzia siku ya kwanza umepata bleed mpaka siku ya mwisho umemaliza ku-bleed
7- Siku za Hatari ni nini?
Siku za Hatari ni siku zote ambazo unaweza kufanya tendo la ndoa na kupata mimba
8- Siku za Uzazi ni zipi?
Siku za uzazi ni zile siku ambazo kwa mtu anayetaka kupata mimba ndio siku zenye uwezekano mkubwa wa kupa mimba, ni siku ambazo dalili zote za yai kutokea au kutoka zinaonekana (kawaida ni siku 3-4)
9- Siku ya Yai Kupevuka au siku ya Mimba
au kutoka katika nyumba yake (ovaries)
Hii ni siku ambayo yai hutoka/hutolewa katika nyumba yake (nyumba ya mayai au ovaries) na kuelekea kwenye mirija ya uzazi ili kushika mimba kwa kiingereza inaitwa ovulation day.
10- KATIKA MAISHA YA KAWAIDA - mwanamke akisema nimeingia kwenye siku zangu basi anamaanisha ameanza bleed. Kama atasema leo niko mwezini siku ya pili basi anamaanisha yuko katika siku ya pili ya hedhi na siku ya pili ya mzunguko wa hedhi.
Kwa hiyo kama mwezi huu wa Sita ulianza kupata hedhi siku yoyote ile basi siku iyo ya kwanza ulipopata hedhi kwa mwezi huu wa sita ndio siku yako ya kwanza ya mzunguko wa hedhi kwa mwezi huu wa sita. Mfano kama ZAYNAB aliingia siku zake tarehe 15/06/2019 basi leo tarehe 24/06 ni siku yake ya 10 ya mzunguko wako wa hedhi. Haijalishi kama alimaliza hedhi yake tarehe 08/06 au kabla ya hapo. Kwa hiyo kitu muhimu hapa ni kuwa siku za mzunguko wa hedhi na siku za hedhi ni vitu viwili tofauti sana. Katika mfano huu hapa ni kuwa Nola leo ni siku yake ya 10 ya mzunguko wa hedhi lakini alimaliza bleed tarehe 08/10 kwa hiyo siku zake za hedhi au siku zake za bleed zilikuwa 4 tu yaani tarehe 05/06, 06/06, 07/06 na tarehe 08/06.
INAENDELEA...... kwenye kipindi kijacho
Dr Ramo +255 712 286 686