Рет қаралды 1,675
USIYO YAFAHAMU KUHUSU NZI.
Fikiria uko LUNCH na Wanchuchu yani Msichana wako
Mrembo na unakaribia kuubugia mshkaki kutoka kwa Babu
JUMA….. Ghafla bin VUUU unaona nzi akikupiga chabo,
akisubiria upepese jicho ili atue kwenye mshikaki wako, cha
kukera zaidi awe ni Yule nzi mwenye rangi ya Dark Blue
inayo Ng’aa kama imepakwa rangi za kumeta meta na
akiyumba kidogo anakuwa kama na rangi ya Ukijani, Huyu
ni maarufu kwa sifa kuu moja, “NI NZI WA CHOONI”.
Basi leo Tumuangazie Kiumbe huyu Mwenye kukera.
Kiumbe mwenye bahati mbaya kwani huchukiwa na kila
mtu nan i chakula mwanana kwa wadudu kama Sisimizi na
Buibui.