Рет қаралды 61,509
EXCLUSIVE: JAMAA ALIYEIBADILISHA DALADALA KUWA MGAHAWA "POMBE MARUFUKU"
Ni Ripoti kutokea Kibaha mkoani Pwani, Camera za Wasafi Digital zimenasa moja ya tukio la ubunifu uliofanywa na fundi wa magari, Shabani Mboga, mkazi wa Visiga kwa Kipofu.
Mboga ameamua kuibadilisha gari ya abiria aina ya DCM iliyokuwa ikibeba abiria kutoka. Mlandizi kwenda Bagamoyo, kuigeuza kuwa mgahawa, jambo ambalo limefanya sehemu yake ya biashara kuwa kivutio kwa watu wengi na wapita njia.
Anasema katika mgahawa huo, ni marufuku kutumia kilevi cha aina yoyote kwakuwa ukiwa ndani ya mgahawa huo unakuwa kama upo juu ya ghorofa, hivyo lolote linaweza kutokea wakati wa kushuka.
@hamisimguta