Рет қаралды 106,529
Bunge limeendelea na mjadala wa kuchangia bajeti kuu ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2022/2023, Mbunge wa Gairo Mhe. Ahmed Shabiby, amesema kitendo cha Serikali kuwakopesha magari watumishi wa Serikali halijafafanuliwa kwa upana hivyo amemtaka Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, atakapohitimisha hoja yake haweze kulifafanua kwa sababu mtumishi anaweza kupunguza safari za kiserikali ili alilinde gari lake lisiharibike.
Pia Mhe. Shabiby, ametoa ushauri kwa Serikali kupunguza gharama za kununua magari ya kifahari kwa Watumishi wa ngazi za chini wawe wanatumia “Double Kibin”, “Prado ndogo” au “Crown” kama Wabunge wanavyotumia “Crown” kwa sababu hela wanazopata Wabunge ni za kununulia “Crown” mpya.
#KutokaBungeni
#HakunaKuleft