Рет қаралды 3,650
Viongozi wa nchi 32 wanachama wa NATO wameanza mkutano wao jana jijini Washington Marekani, ambapo katika hotuba ya ufunguzi wa mkutano huo, Rais Joe Biden wa Marekani alisema kuwa nchi wanachama wa NATO wataipatia Ukraine mitambo mitano ya kimkakati ya ulinzi wa anga.
Biden amesema Marekani kwa kushirikiana na nchi za Ujerumani, Italia, Uholanzi na Romania wamekubaliana kuipatia Ukraine mitambo ya kisasa ya kimkakati ya ulinzi wa anga aina ya Patriot ili kuiwezesha nchi hiyo kukabiliana na mashambulizi ya anga ya majeshi ya Urusi.
Mitambo ya uliniz ya anga ya Patriot inatajwa kuwa ni yenye teknolojia ya hali ya juu ya ulinzi wa anga. Ina uwezo wa kuzuia makombora adui, mashambulizi ya ndege vita na ndege zisizo na rubani kutoka eneo la umbali mrefu.
Unaweza kutufuatilia kupitia;
TWITTER: / thechanzo
INSTAGRAM: / thechanzo
FACEBOOK: / thechanzo
TIKTOK: www.tiktok.com/@thechanzo?is_...
Au tembelea tovuti yetu: www.thechanzo.com
Je, una habari? wasiliana nasi kupitia Telegram/WhatsApp +255 753 815 105
The Chanzo Initiative, 2024 © All Rights Reserved.