Рет қаралды 12,889
Maziwa ni chakula kinachopatikana kutoka kwa wanyama. Binadamu tunakunywa maziwa ya ng'ombe mbuzi ngamia nk.
Maziwa asilia ambayo hayajachachuliwa naamanisha yaliyota moja kwa moja kwa ng'ombe huwa yana protini,mafuta vitamins (A,D,E) pia huwa yana madini ya Chuma yanayo saidia kutengeneza damu,Madini ya calcium ambayo hutusaidia kuimarisha mifupa. Haya maziwa yenye viambata hivi huitwa MAZIWA ASILIA (Full fat milk)
Maziwa ya kisasa ni yale yanayotokana na maziwa asili. Ila yamechujwa mafuta na unapokuwa unachuja mafuta unazichuja pia vitamin zinazotembea na mafuta kama vitamin A,D,E na baada ya hapo utalazimika kuweka Vitamin Feki ambazo tunasema ni "Artificial vitamin" ili kumdanganya mtumiaji kwamba zile vitamin ulizotaka kwenye maziwa teknolojia hii ya kuchuja haijazipoteza. Kumbe zimeongezwa nyingine ambapo zile asilia zimepotea.
Maziwa ambayo ni Skimmed milk ubaya wake wa kwanza huwa hayana ladha, Pili yana uwezo mkubwa wa kupandisha sukari kuliko maziwa asili, tatu hayawezi kukusaidia kudhibiti uzito wako ina maana yatakuhatarisha kupata maradhi mengi yatokanayo na kisukari kutodhibitika na uzito kutodhibitika.
Hebu tizama Video hii mpaka mwisho utaelimika.
Pata nakala ya sayansi ya mapishi upate kujinoa na nina uhakika utayavuka mateso yote unayo pitia kiafya endapo ukifuata elimu hii kwa mazingatio ya hali ya juu.