Рет қаралды 50,837
Banda Bora la Kuku wa Nyama | Kuku wa Mayai | Kuku Chotara
Kujenga Banda Bora
Banda bora ni banda ambalo linakidhi mahitaji ya kuku wako na liendane na idadi ya kuku unaofuga.
Sifa za banda bora.
I. Lijengwe sehemu isoyotuama maji
II. Likinzane na uelekeo wa upepo na mvua
III. Liruhusu mzunguko wa hewa
IV. Liwakinge kuku wako dhidi ya baridi
V. Liwe na vichja kwaajili ya kupumzika, kufanya mazoezi na kulala, pia Liwe na viota vya kutagia ambavyo huwekwa kuku wakifikisha miezi 3
VI. Liwe rahisi kusafishika
VII. Liendane na idadi ya kuku bandani
Hapa sasa watu wengi hua wanafeli na kujisababishia changamoto za magonjwa, kudonoana na kula mayai.
Kuku anahitaji sehemu ya kutosha ili aweze kuwa huru na kufanya mazoezi ndio maana wanaofuga huria au nusu ndani nusu nje wanapata matokeo mazuri.
Kila aina ya kuku anahitaji nafasi yake.
1m square inahitaji kuku chotara 4/5
1m square inahitaji kuku wa mayai 6/8
1m square inahitaji kuku wa kienyeji/nyama 8.
Mfano unataka kujenga banda la kuku chotara 100, unachukua 100÷4=25m square au 100÷5=20m square, sasa hii 25/20m square ndio ukubwa wa banda. 25=6.25x4 na 20=5x4.
Ukizingatia vipimo utapunguza changamoto.