Рет қаралды 2,550
Yapo mengi usiyoyajua kuhusiana na biashara ya mboga mboga na matunda, wapo ambao wamefanikiwa kwa kihasi kikubwa hata wakaweza kununua magari, viwanja, kujenga na wanasomesha watoto shule nzuri kupitia biashara hii.
Lakini pia kuna changamoto zake, mchakato wa kupata matunda bora kuyatunza na kuyauza kwa wapita njia sio kazi rahisi. Wengi wao hutumia usiku mzima kutafuta matunda muda ambao watu wengi wempumzika wao wanakuwa barabarani kutafuta mbogamboga na matunda ili waweze kuwauzia wateja vitu vilivyo fresh.
Leo hii VOAG kupitia kipindi chake cha Masoko Yetu imemtembelea Bw. Salum Magembe na kusikiliza story yake kuhusiana na biashara hii ya mbogamboga na matunda kwani ndiyo kazi pekee inayomuweka hapa mjini na kwa muonekano tu inaonekana kwake mambo sio mabaya sana; hebu tumsikilize.