Рет қаралды 18,322
Uwekezaji katika mifuko ya pamoja ni rahisi kuliko unavyofikiria. Ni njia nzuri ya kukuza mtaji kwa wale wenye malengo ya muda mfupi, kati na ya muda mrefu.
Mifuko hii ni aina ya uwekezaji wa pamoja ambayo inaruhusu wawekezaji walio na malengo sawa kuwekeza fedha zao kwa pamoja kwenye jalada la dhamana au mali zingine.
Wawekezaji (wenye vipande) hawamiliki dhamana hizo za mfuko moja kwa moja. Umiliki wa mfuko umegawanywa katika umiliki wa vipande. Kadiri mfuko unavyoongezeka au kupungua kwa thamani ndivyo thamani ya kipande huongezeka au kupungua ipasavyo. Idadi ya vipande inategemea bei ya ununuzi wa kipande,wakati wa uwekezaji na kiwango cha pesa kilichowekezwa.
Kawaida, faida ya uwekezaji kwa wamiliki wa vipande hupatikana kwa mfumo wa gawio la mapato na kukua kwa mtaji, inayotokana na uwekezaji wa pamoja. Kila kipande kinapata mapato sawa, yaliyotokana na kiwango kilichowekezwa kama mtaji katika kipindi chochote.
Uwekezaji katika mifuko ya uwekezaji wa pamoja, huhamisha utaalam wote wa uwekezaji kwa wale wenye uwezo wa kusimamia masuala ya uwekezaji na hao ndiyo sisi, UTT -AMIS (Wasimamizi wa Mfuko)
soma zaidi
"Uwekezaji wa pamoja kwa muhtasari | DHAMANA YA UWEKEZAJI NA USIMAMIZI RASILIMALI TANZANIA" www.uttamis.co.tz/sw/uwekezaj...