RAIS DKT. MAGUFULI AWASIMAMISHA TBA KUJENGA NYUMBA ZA MAGEREZA UKONGA

  Рет қаралды 116,137

Ikulu Tanzania

Ikulu Tanzania

5 жыл бұрын

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 16 Machi, 2019 amefanya ziara ya kushtukiza katika mradi wa ujenzi wa nyumba za makazi ya Askari Magereza wa gereza la Ukonga Jijini Dar es Salaam na kuagiza mradi huo ukabidhiwe kwa Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ).
Mhe. Rais Magufuli ametoa maagizo hayo baada ya kubaini kuwa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) imeshindwa kutekeleza mradi huo kwa wakati, licha ya Serikali kutoa shilingi Bilioni 10 za ujenzi.
Ametaka wataalamu wa TBA waliokuwa wakisimamia mradi huo pamoja na Askari Magereza waondoke na kuwapisha JWTZ.
“Kwa hiyo hapa nisimuone mtu wa TBA, nisimuone mtu wa Magereza kuja kusimamia, muwaache Jeshi la Wananchi wafanye kazi zao, siku watakapokuja kunikabidhi na mimi nitawakabidhi Magereza, kwa hiyo watu wa TBA kuanzia leo nimewafukuza hapa” amesema Mhe. Rais Magufuli.
Mhe. Rais Magufuli ameelezea kutoridhishwa na utendaji kazi wa TBA katika mradio huo ambao ulianza zaidi ya miaka 2 iliyopita kwa kushirikisha Jeshi la Magereza ambalo lilikuwa linaisadia TBA katika kazi za ujenzi, na ametaka TBA na Jeshi la Magereza wabadilike katika utekelezaji wa majukumu yao.
“Nataka kila mlipo watu wa Magereza mfanye kazi, msimamie watu, kama ni ng’ombe muwafuge vizuri wazalishe vizuri hadi muuze mazao nje, kama ni kilimo mlime kwelikweli, muwe ni jeshi la kuzalisha, hii ni aibu kuleta jeshi jingine la wananchi kuja kuwajengea nyumba nyinyi, wakati nyumba mnakaa nyinyi, mlitakiwa muwe mmeshapanga mkakati kwamba TBA wamesuasua, ngoja tufyatue matofari, tuanze kujenga” amesisitiza Mhe. Rais Magufuli.
Mkuu wa Utawala wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Kanali Charles Mbuge amesema JKT itakamilisha ujenzi huo ndani ya kipindi cha miezi 2 na nusu kuanzia kesho na kwamba kazi zitafanywa usiku na mchana.
Aidha, Mhe. Rais Magufuli ameitaka TBA kutoa maelezo ya namna fedha zilizotolewa na Serikali kiasi cha shilingi Bilioni 10 zilivyotumika, na ameonya kuwa endapo itabainika matumizi ya fedha hizo hayaendani na kazi zilizofanyika hatua kali zitachukuliwa.
Katika mradi huo, ujenzi wa majengo 12 ya makazi ya Askari Magereza yaliyopangwa kuwa na ghorofa 4 kila moja ulioanza Desemba 2016 umefikia asilimia 45 tu na unaendelea kwa kusuasua.

Пікірлер: 82
@abduladhimually3542
@abduladhimually3542 5 жыл бұрын
Jembeeee#watakubalitu..........your a good leader never met before
@nyanda427
@nyanda427 5 жыл бұрын
Waoh. Love you Mr. President Dr. John Pombe Magufuli
@sk-wj9or
@sk-wj9or 5 жыл бұрын
I salute you Mr president!
@amos878
@amos878 5 жыл бұрын
Outstanding mkuu na waje walale na wafungwa wao 😂😂😂😂
@olembetonga7341
@olembetonga7341 24 күн бұрын
😂😂
@allyfutto8763
@allyfutto8763 5 жыл бұрын
Faraja iliyoje kubahatika amirijeshi anayeona mbalisana watanzania ni jambo la kujivunia sana ni mipango ya mungu Tumeteseka sana Tubadirike twende na wakati.
@freddymello3227
@freddymello3227 5 жыл бұрын
Sifa ya kiongozi bora ni kuchukua hatua katika muda mwafaka. hongera J.P.M kwa hatua hii uliyochukua.hakika wewe ni mfano wa kuigwa kwa vizazi vijavyo. aina ya uongozi wako ni wito na kujitoa kweli kweli.nchi yetu inauozo kila sehemu. Viva C.C.M,viva J.P.M
@user-pe1ze9sw4f
@user-pe1ze9sw4f 10 ай бұрын
Uko ulipo Mungu azidi kukulinda
@aloycekiwia8613
@aloycekiwia8613 5 жыл бұрын
Hata Umchukie vipi Uncle Magu, Kuna mambo mengine lazima umkubali tu! labda uwe Chizi.!? Hizi nyumba nazikumbuka ni miaka mingi kweli. Kumbe walishapewa na Pesa zote.!!??
@kwandukanunda4351
@kwandukanunda4351 5 жыл бұрын
Watapike
@shabanmlekwa9513
@shabanmlekwa9513 5 жыл бұрын
Na Tanzania ndo ilishafikia hapo. Alitakiwa aje mtu ka Magufuli.
@neemajoshuaer9562
@neemajoshuaer9562 5 жыл бұрын
Saf Sana mhe Rais
@freddymello3227
@freddymello3227 5 жыл бұрын
Neema Joshuaer ,mambo!!uko poa neema wng
@bundalamlolasa3774
@bundalamlolasa3774 5 жыл бұрын
Safe Sana mheshimia Rais Kaz yako inaonekana.
@mohdsalum3832
@mohdsalum3832 5 жыл бұрын
Safi sana
@ramadhanimmana3829
@ramadhanimmana3829 5 жыл бұрын
Safi saan mkuu
@zefamange7281
@zefamange7281 5 жыл бұрын
KMBIZA HAO COMMANDO WANGUUU, WAMEZOEA UJINGA UJINGA HAO
@JoasDioniz
@JoasDioniz 5 жыл бұрын
Haaaaahaaaaa lazima wazitapike #JeshiHalishindwi #TanzaniaMpyaYaJPM
@magilemabula5755
@magilemabula5755 5 жыл бұрын
Tanzania kwanza
@shukurumwangosi1537
@shukurumwangosi1537 5 жыл бұрын
Wooh
@victustemba
@victustemba 5 жыл бұрын
Hapa kazi tu, 10% watazitapika..!😀
@gooddeeds162
@gooddeeds162 5 жыл бұрын
Victus temba Shemeji Nafurahi sana hatua anazochukua Mh Rais zinatia sana Faraja, Lakini Kuna wachache wanataka kuzingua tu . Watashindwa tu
@jacksonjombo7221
@jacksonjombo7221 5 ай бұрын
God give me a vision like this Father, Ee Mungu nipe maono kama uyu Baba
@j.bjacobbasubi2187
@j.bjacobbasubi2187 5 ай бұрын
I'm a congolaise but 😢😢😢
@amirimbago8325
@amirimbago8325 5 ай бұрын
Nikikupa maono watakuua mapema...pambanatuu na hali yako kwa maendeleo ya ukoo wenu.
@masigomhoja5182
@masigomhoja5182 5 жыл бұрын
Safi sana duh kura yangu mimi ni yakoo mjombaa
@zawadix9574
@zawadix9574 5 жыл бұрын
Jembe
@agneomasonda2462
@agneomasonda2462 5 жыл бұрын
Piga kazi baba
@pacomezouzoua9175
@pacomezouzoua9175 10 күн бұрын
Chuma kweli kweli daah Why God ulimchukua mapema 😢
@tanzania2559
@tanzania2559 5 жыл бұрын
🙌🏾🙌🏾🙌🏾👏🏾👏🏾👏🏾👏🏾👏🏾
@shayoyahaya3736
@shayoyahaya3736 5 жыл бұрын
Sipata ona...!! Huyu ni zaidi ya Rais. Washa moto haya ndio mabadiliko ... Walishazoea ubwenyenye....
@tufyambefredrick4340
@tufyambefredrick4340 5 жыл бұрын
Ukimuona mh Raisi amevaa hiyo kofia na yuko kwe ziara ujue kuna jambo litatokea nani anakubali hii
@RedpilledPhoenix
@RedpilledPhoenix 5 жыл бұрын
Mungu mlinde Rais wa 🇹🇿 namwombea afya nzuri
@kahmardintebe9266
@kahmardintebe9266 7 ай бұрын
Chuma hakika mungu alituzawadia Ila hatukuona umuhimu wake pumzika kwa amani jpm
@benbranco3688
@benbranco3688 3 жыл бұрын
R.I.P MKUU DAHH
@gabrieladam491
@gabrieladam491 5 жыл бұрын
Huwa nakuelewaga Sana naomba Mungu anipe nifanye kama wewe President
@Lusekelo98
@Lusekelo98 Ай бұрын
Real life
@h2kizzyboymsafi832
@h2kizzyboymsafi832 5 жыл бұрын
Safi sana jembe
@joesimba
@joesimba 2 жыл бұрын
2:50
@ismailyusuph740
@ismailyusuph740 5 жыл бұрын
....NA WATAITAPIKA...! JESHI halishindwi Mh Rais...!
@matingo-bk1248
@matingo-bk1248 5 жыл бұрын
Hii ndio maana halisi kiongozi, kuwa na maamuzi magumu mambo yanapoenda sivyo
@mupagedragon1972
@mupagedragon1972 3 жыл бұрын
Vizur sana baba etu magu
@nassoromzenga866
@nassoromzenga866 5 жыл бұрын
Napenda sana mamuz ya rais anataka wachapa kaz
@allythabit5175
@allythabit5175 5 жыл бұрын
raha sana
@maduhansanga109
@maduhansanga109 5 жыл бұрын
Nakukubali sana rais wetu
@goodlegacytv5068
@goodlegacytv5068 14 күн бұрын
Duh mwamba kabisa
@godfreymwacha8711
@godfreymwacha8711 5 жыл бұрын
That my president I salute you
@mussamkali9926
@mussamkali9926 8 ай бұрын
Magu kazini
@manyotaskipper5765
@manyotaskipper5765 5 жыл бұрын
Ukinuna UWE NA SABABU MJOMBA MAGU BADO WANAJUSAHAU TBA WANALALA TU
@utukufueliya5279
@utukufueliya5279 5 жыл бұрын
kwa kauli hii kuna watu wanaenda kufungwa.....
@ulemse6067
@ulemse6067 5 жыл бұрын
Twahitaji kiongozi Kama huyu huku Kenya.
@kolinsimahanga9845
@kolinsimahanga9845 5 жыл бұрын
jwtz safi
@thomasmollel9465
@thomasmollel9465 4 ай бұрын
Rest in peace kipenzi cha watanzania
@utukufueliya5279
@utukufueliya5279 5 жыл бұрын
Kazi usiku na mchana.... 😀😀😀😀😀😀
@charlesmakuri792
@charlesmakuri792 5 жыл бұрын
Hawa wanajikosha kwa kina mbowe eti serikali iwape magodolo wafungwa,hivi uende gerezani utoke hujakelwa sasa hereza au umeenda kutalii ,jengeni makazi yenu
@barakamashinga463
@barakamashinga463 5 жыл бұрын
A cleansheet president!
@mickwealthy500
@mickwealthy500 Жыл бұрын
RIP
@user-me2nk2me9d
@user-me2nk2me9d 6 ай бұрын
Jaman ludi kigambon uvukaji feery tunateseka panton kla sku zinaalibika tunateseka
@samsonmagesa3959
@samsonmagesa3959 5 жыл бұрын
Hapo ndipo waga Nasema 2020 Kura yangu Kwakoooooo
@samsonmagesa3959
@samsonmagesa3959 5 жыл бұрын
Jeshi halishindwi huko Vizuri Kanali
@raphaelkessy7360
@raphaelkessy7360 4 ай бұрын
Pumzika kwa amani na baraka Kamanda mkuu JPM
@Mwinamila-3
@Mwinamila-3 6 ай бұрын
N viongoz wachache wanaoweza kichukua maamuzi kama haya
@genimaige6023
@genimaige6023 5 жыл бұрын
kusema ukweli toka moyoni jeshi la magereza lijitathinini upya yani ni sawa na baba tkt nyumba anatoa maagizo ktk familia yake na hayatekelezeki kwa wakati, hata mm nimechukia hii ni aibu, kama pesa zipo tatizo ni nn?? 😄😄😄😄😄😄
@tevintevin1884
@tevintevin1884 5 жыл бұрын
Hadi raha ...bravo Mr President... Hao wa kuzitapika itabidi watapike mpaka nyongo
@jamessanga2176
@jamessanga2176 5 жыл бұрын
hahahahahah
@vincentmasanja789
@vincentmasanja789 5 жыл бұрын
Inawezekana Raisi wa awamu hii akaweka historia ya pekee ,kwa kuwa nchini bila kwenda ughaibuni kwa miaka minne.
@fathermore9772
@fathermore9772 5 жыл бұрын
Vincent Masanja tuseme asante kwakua nakiongozi mwenye mtizamo chanya namsimamo kama uncle
@vincentmasanja789
@vincentmasanja789 5 жыл бұрын
Hakika Fadher More.
@ismailmasoud6001
@ismailmasoud6001 Ай бұрын
Aisee huyu jamaa alikua ni MWAMBA kabisa..!
@thabitngangila8562
@thabitngangila8562 5 жыл бұрын
chuma cha pua ukizingua anakuumbua
@athumanomary1438
@athumanomary1438 5 жыл бұрын
Ewe mwenyez MUNGU ewe mwenyez MUNGU tunakuomba na tunazidi kukuomba enderea kumuongoz kumsimamia kumrinda na kuzidi kuimarisha afya yake raisi wetu ewe mwenyez MUNGU mkuu
@user-mf8iu1qp3n
@user-mf8iu1qp3n 4 ай бұрын
Hahahaha et ntawakabidhi 😂😂 walale na magereza wao😂😂 Rest in peace 🕊️ rais wetu
@eliyawilliammagesamarwa8413
@eliyawilliammagesamarwa8413 5 жыл бұрын
Kura yangu
@florencebudoya3814
@florencebudoya3814 5 жыл бұрын
Elelo yeye.
@lengaiolesabaya8209
@lengaiolesabaya8209 5 жыл бұрын
Mungu unatisha.Unajua kuwaleta watu wako kwa saa zako, kuliponya taifa lako.
@samuelmwaikambo5691
@samuelmwaikambo5691 5 жыл бұрын
President JPM nadhani bado hawajakuelewa hao wanafanya wajuavyo ni pingu tu huko ni kuhujumu mali ya watanzania walipa kodi usiku na mchana.
@abdilahijuma2852
@abdilahijuma2852 5 жыл бұрын
Dr magufuli safi sana
@mashimbadeograthiasmathias8583
@mashimbadeograthiasmathias8583 5 жыл бұрын
Canal jenga Bila shida Ila hao MAGEREZA watapike hela hizo
@SaleheMkomwa
@SaleheMkomwa Ай бұрын
Fukuza tu
@mussaramadhani-in1ci
@mussaramadhani-in1ci Жыл бұрын
Zmzm
JPM ALIVYOWAKA KUHUSU MAKONTENA KUCHELEWA
8:38
Millard Ayo
Рет қаралды 350 М.
HOW DID HE WIN? 😱
00:33
Topper Guild
Рет қаралды 44 МЛН
WHO LAUGHS LAST LAUGHS BEST 😎 #comedy
00:18
HaHaWhat
Рет қаралды 20 МЛН
I Can't Believe We Did This...
00:38
Stokes Twins
Рет қаралды 104 МЛН
Каха и суп
00:39
К-Media
Рет қаралды 5 МЛН
BREAKING: JPM Atembelea Shule Aliyosoma Nyerere
13:30
Global TV Online
Рет қаралды 236 М.
Rais Magufuli afanya ziara ya kushtukiza Terminal One JNIA Mei 13,2016
17:24
Captain Aliyetoroka na NDEGE Kenya Apewa Mamilioni na JPM!
5:25
Global TV Online
Рет қаралды 498 М.
RAIS MAGUFULI ALIVYOKWENDA BENKI KUU BILA KUWATAARIFU
8:03
Millard Ayo
Рет қаралды 1,9 МЛН
HOW DID HE WIN? 😱
00:33
Topper Guild
Рет қаралды 44 МЛН